Monday, 14 July 2014

Kiwanda cha 'Samsung' chatumikisha watoto





Kampuni ya bidhaa za elektroniki ya, Samsung imesema kuwa imepata ushahidi wa kuwatumikisha watoto kinyume na sheria katika moja ya kiwanda cha kusambaza bidhaa zake nchini China cha Dongguan Shinyang .
Samsung imesema kuwa iliichunguza kampuni hiyo baada ya madai kutoka kwa shirika la kupambana dhidi ya utumkishaji wa watoto ya Marekani 'China Labor Watch' kuituhumu kwa kuwatumikisha watoto.
Awali kampuni hiyo ya korea kusini ilikana kwamba baadhi ya kampuni zinazosambaza bidhaa zake zinawaajiri wafanyakazi walio chini ya umri wa miaka 16,lakini uchunguzi uliofanywa na shirika hilo umeilazimu kampuni hiyo kukiri makosa yake.

Takriban watoto watano walio chini ya umri wa miaka 16 walikuwa wakitengeneza baadhi ya sehemu za simu za samsung ,kulingana na uchunguzi wa siri wa shirika hilo la haki za wafanyikazi,lililo na makao yake mjini New York.
Watoto hao ambao wamekuwa wakifanya kazi bila kandarasi wamekuwa wakilipwa thuluthi mbili za mshahara wa mtu mzima.

Wasambazaji wa bidhaa za Samsung wanashtumiwa kwa kuvunja sheria za kazi za uchina kupitia kuwaruhusu watoto wadogo kufanyakazi katika kemikali mbali na kupuuza sheria za uchina kuhusu kazi za mda wa ziada ambapo hufanya kazi kwa masaa 11 katika zamu ya masaa 10.

Hivi majuzi kampuni ya samsung ilitoa matokeo ya ukaguzi wake kuhusu wasambazaji wa bidhaa zake nchini Uchina ambayo hayakupata ushahidi wowote kuhusu ajira ya watoto.
kampuni hiyo imeahidi kukata uhusiano wake na kampuni za usambazaji wa bidhaa zake iwapo itathibitisha madai hayo mapya

Shinikizo wasichana kuachiliwa Nigeria





Malala na mmoja wa wazazi wa wasichana waliotekwa nyara Nigeria

Mwanaharakati mwenye umri mdogo raia wa pakistan Malala Yousafzai anatarajiwa kukutana na rais wa Nigeria Goodlack Jonathan mjini Abuja hiii leo kushinikiza kuchukuliwa hatua zaidi ili kuwakoa wasichana wa shule waliotekwa na kundi la wanmgambo wa Boko Haram mwezi April.

Tayari mwanaharakati huyo ashakutana na familia za wasichana hao kuonyesha uzalendo wake kwao.
Boko Haram wametoa kanda ya video ya kusuta kampeni za kutaka kuachiliwa wasiha hao mabpo kundi limetaka kuachiliwa kwa wapiganaji wake.

Malala alipigwa risasi kichani na kundi la Taliban nchini Afghanistan alipokuwa akipigania elimu kwa wasichana

Monday, 23 June 2014

Wandishi wa Al Jazeera miaka 7 jela


Mahakama nchini Misri imewahukumu jela miaka saba wandishi watatu wa habari wa shirika la habari la Al Jazeera waliokuwa wamezuiliwa kwa miezi sita nchini humo.

Walipatikana na hatia ya kueneza habari za kupotosha na kushirikiana na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Muslim Brotherhood.

Mmoja wa wandishi hao ni Peter Greste, raia wa Australia na ambaye pia alikuwa mwandihi wa habari wa BBC wakati moja.

Thursday, 12 June 2014

Blatter Ataka muhula wa tano urais Fifa



Blatter adokeza nia yake kutaka urais wa Fifa kwa muhula wa 5.
Rais wa shirikisho la kanda FIFA, Sepp Blatter, amesema yuko tayari kuendelea na wadhfa huo kwa muhula mwengine wa 5.
Akizungumza katika kikao maalum cha Fifa huko Sao Paulo amesema yuko tayari kugombea tena cheo hicho kama rais wa shirikisho hilo kubwa linalosimamia soka ya dunia.
Kwa kutangaza hivyo ni kwamba amepuuzilia mbali kauli za maafisa wa soka wa Europa wanaomtaka ajiuzulu kufuatia madai ya rushwa yanayoiandama Fifa,wakati ilipochaguliwa Qatar kuwa mwenyeji wa kombe la dunia 2022.
Europa imemtaka Blatter ajiuzulu kufuatia tuhuma za rushwa katika Fifa.
Awali Blatter mwenye umri wa miaka 78 alikuwa amedokeza kuwa angestaafu baada ya kipindi chake cha sasa.
Blatter pia amependekeza kuwa mameneja wa timu waruhusiwe kutafuta haki pale kwa kutumia technologia pale watakapohisi maamuzi ya refa hayakuwa sawa.
Tisho la Maandamano
Wakati huo huo watu 10 wameripotiwa kukamatwa na kupelekwa vituo vya polisi huko Rio de Janeiro ili kuhojiwa kuhusiana na kushiriki kwao katika maandamano yenye ghasia.
Ulinzi unaendelea kuimarishwa hasa katika miji ya Sao Paulo na Rio ambako baadhi ya makundi ya watu wametishia kufanya maandamano kudai maslahi yao, wakati wa ufunguzi wa kombe la dunia utakaofanyika chini ya saa 24.

Ulaya wataka Blatter ajiuzulu kwa usemi



Rais wa Shirikisho la kandanda duniani, FIFA, Sepp Blatter.
Maafisa wa kandanda wa Europa sasa wamemtaka rais wa shirikisho la kimataifa la kandanda FIFA, Sepp Blatter, ajuzulu kutokana na madai ya rushwa yanayoindama Fifa.
Wametilia shaka uongozi wake.
Mkuu wa chama cha soka cha uholanzi Michael Van Praag, amesema chini ya uongozi wa Blatter ,Fifa imeandamwa na tuhuma za rushwa na ili Fifa kujisafisha ni sharti Blatter angatuke.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha soka Uingereza , Greg Dyke,amesthtumu kauli ya Blatter kuwa madai ya rushwa kuhusiana na kuchaguliwa kwa Qatar kuwa mwenyeji wa kombe la dunia 2022 yanayoripotiwa katika magazeti ya Uingereza yamechochewa na ubaguzi wa rangi.
Blatter anatarajiwa kutangaza nia yake ya kuwania nafasi kipindi cha tano kuingoza Fifa katika uchaguzi wa Fifa unaotarajiwa kufanyika mwaka ujao.
Kwa sasa wajumbe wa Fifa wanavikao huko Sao Paulo wakijiandaa kwa ufunguzi wa kombe la dunia hapo kesho ambako Sepp Blatter pia amekuwa akitoa cheche za maneno dhidi ya wale wanaoisema vibaya Fifa na Qatar.

Tisho la mgomo Uwanja wa ndege Rio


Makundi mbalimbali yamekuwa yakitumia ujio wa kombe la dunia kugoma kudai maslahi yao
Wafanyakazi wa kiwanja cha ndege cha Rio wametangaza mgomo wa saa 24 kuanzia usiku wa manane saa za Brazil.
Hii ni kumaanisha mgomo huo utaendelea hadi wakati wa ufunguzi wa kombe la dunia.
Japo sherehe na mechi ya ufunguzi zinafanyika mjini Sao Paulo, na ni asilimia 20% tu ya wafanyikazi ndio watakao goma, mgomo huo bila shaka utatatiza usafiri katika mji huo wa Rio ulio wapili kwa ukubwa nchini Brazil.
Wafanyikazi wanaoshughulikia abiria na mizigo na wale wanaofanya usafi wa hata ndegeni ni baadhi ya watakaogoma.
Afueni baada ya baadhi ya wabrazil wafanyikazi wa reli na mabasi kusitisha migomo ya kudai posho.
Sehemu za kuhudumia wageni wa kimataifa na wa ndani ya nchi zitatatizwa na mgomo huo.
Wafanyikazi hao wanadai nyongeza ya mshahara na posho za kufanya kazi wakati wa kombe la dunia wakisema kazi zimeongezeka.
Mmoja wa viongozi wa chama cha wafanyikazi hao , Luiz Braga, amekana wanatatiza kombe la dunia kwa maksudi, akieleza kuwa 'hatutaki kuharibu kombe la dunia, tunachofanya ni kudai haki zetu tu'.

Nchi za Afrika Mashariki kusoma bajeti

 
Serikali ya Rais Museveni inategemea kipato chake zaidi kutoka mkusanyo wa kodi
Bajeti katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinatarajiwa kutangazwa. Ni wakati ambapo mizani ya matumizi na mapato ya serikali huanikwa hadharani.
Biashara katika Jumuiya imekuwa mhimili imara wa uchumi wa nchi ya Uganda kukua, licha ya msukosuko katika masoko ya dunia.
Nchini Kenya wananchi wanatarajia kuwa bajeti itaweza kuwalinda kutokana na mfumuko wa bei pamoja na kiwango kikubwa cha kodi inayotozwa.
Hali ni hiyo hiyo nchini Uganda kwa mujibu wa mwandishi wetu wa Kampala Ali Mutasa.
Kiokozi cha Uganda kiuchumi, kwa mujibu wa Rais Yoweri Museveni - ni Kilimo, Viwanda, Huduma, na Tetama - yaani, teknolojia ya taarifa na mawasiliano (ICT).
Katika sekta hizo zote nne, mali huzalishwa na nafasi za kazi hubuniwa. Hivyo bajeti ya mwaka 2014/15 itamakanikia sekta hizo nne.
Mwaka huu wa fedha, ingawaje, wafadhili waliikatia misaada bajeti - karibu robo.
Uganda ilipitisha sheria kali zaidi dhidi ya wapenzi wa jinsia moja
Si kwa sababu za kiuchumi, bali za kisheria; Uganda ilipoamua kupitisha sheria kali zaidi dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.
Labda bajeti itaongelea kirefu athari ya kukatwa msaada huo.
'Faida ndogo, kipato kidogo'
Kipato cha serikali zaidi kinatokana na kodi. Zaidi ya thuluthi mbili mwaka huu wa fedha serikali ikitegemea mkusanyo wa kodi, zaidi ya trilioni 8.
Lakini kukazuka tobo la kama $milioni 148, sababu ya baadhi ya makampuni kushindwa kulipa kodi.
Mojawapo ya sababu ni vita vya Sudan Kusini ambavyo vilivuruga biashara na Uganda, iliokuwa karibu $1bn, kila mwezi.
Uchumi haukukua kwa karibu 7%, badala yake ulizidi 5%, hii ikimaanisha faida za makampuni fulani zilikuwa chini hivyo kipato cha serikali kupungua.
Shilingi ya Uganda imeshuka dhidi ya sarafu kama dola ya Marekani
Sekta binafsi ambayo inatiliwa shime na serikali pia inatapatapa kutokana na gharama kubwa ya mikopo, kwani kima cha riba ya benki kuu kikoo juu sana, 11%, na kuifanya mikopo katika benki za kibiashara kuwa ghali mno kwa wafanyabiashara wengi wadogowadogo, ambao ni mhimili wa uchumi.
'Kupanda kwa gharama ya maisha'
Thamani ya shilingi iko chini kulingana na fedha ngumu kama dola, na hivyo kuyafanya maagizo kuwa ghali zaidi, mfano petrol au magari ambayo huagizwa kutoka nje.
Matokeo yake ni nauli kuwa juu na bei za vitu kupanda, japo serikali inasema inadhiiti vyema mfumko wa bei ambao uko kasoro ya 6%.
Ingawaje serikali ya Uganda, inatazamia mafuta kuanza kuuzwa mwaka huu wa fedha, huenda ikaamua kugharamia matumizi yake muhimu si kwa kupandisha zaidi kodi, bali kwa kupata mikopo katika masoko ya fedha ndani na nje ya Uganda.
Kwa mfano, mikopo inachangia kasoro ya 30% ya zao ghafi la ndani Uganda - ni kiwango cha chini, kulinganisha na Kenya 50% na Tanzania 40% hivi.
Ingawaje, mfuko wa fedha wa kimataifa, IMF na Benki ya Dunia na wadeni wengine wataiwasa Uganda isiandame mkondo huo wa madeni.

Kumekucha Brazil, Dimba kung'oa nanga








Michuano kuanza Brazil

Kombe la dunia Brazil 2014 linatarajiwa kungo'a nanga baadaye leo jioni huku Brazil na Croatia wakitoana kijasho mjini Sao Paolo.

Dimba hilo litakalodumu kwa mwezi mmoja, litashuhudia mataifa 32 yakimenyana kuwania kombe hilo katika fainali itakayochezwa mjini Rio tarehe 13 Julai.





Mechi ya ufunguzi itaanza baada ya sherehe ya kufungua mechi hiyo mjini Sao Paulo. Ni mechi ambayo itakuwa inatoa kipaombele kuonyesha umuhimu wa kukuza vipaji, utu na kabumbu.

"wacheni niwambie kuwa wakati umewadia. Tunaenda sote . Hili ni kombe letu la dunia, '' alinukuliwa akisema kocha wa Brazil Luis Felipe Scolari.

Mwaka jana zaidi ya watu milioni moja walishiriki katika maandamano ya kupinga hatua ya serikali kuandaa michezo hiyo kwa gharama ya juu wakati wananchi wengi wakiishi kwa umasikini.

Serikali ya Brazil iko makini kuzuia kutokea tena kwa ghasia zilizoshuhudiwa wakati wa maandamano hayo. Rais Dilma Rousseff amesema kuwa hatakubali kamwe maandamano yanayosababisha ghasia kuathiri kombe la dunia.

Maelfu ya polisi na wanajeshi watashika doria nchini humo kuhakikisha kuwa mechi zinafanyika bila vurufu.

England itacheza mechi yao ya ufunguzi dhidi ya Italy Jumamosi tarehe 14 , mechi ambayo itapeperushwa moja kwa moja na BBC.

Timu hiyo pia itacheza dhidi ya Uruguay na Costa Rica katika kundi D.

Wenyeji Brazil wataanza mechi leo wakipigiwa upatu kushinda kombe la dunia kwa mara ya sita wakati mabingwa watetezi Hispania nao wanakilenga kushinda kombe hilo kwa mara ya nne baada ya kushinda ubingwa wa Ulaya miaka miwili iliyopita.

Monday, 9 June 2014

Uwanja wa ndege washambuliwa Pakistani



Wanajeshi wa Pakistan wakiwa kwenye uwanja wa ndege wa Karachi kukabiliana na washambulizi.
Mapambano ya risasi yaliyodumu saa tano katika uwanja wa mji mkubwa zaidi nchini Pakistani ,Karachi yamewauwa watu 23 wakiwemo washambuliaji wote 10.
Washambuliaji hao waliokuwa na silaha nzito nzito waliingia sehemu ya majengo ya uwanja huo kupitia njia zinazotumiwa na ndege za mizigo au zile zinazotumiwa kuwapokea wageni wenye hadhi na sifa yaani V.I.Ps.
Walipenya usiku wa manane na kuanza kuwashambulia maafisa usalama kwa gruneti na kwa kuwafyatulia risasi.
Makamanda katika jeshi waliitwa kukabiliana na washambuliaji hao na milio ya risasi ilisikika hadi alfajiri wakati hali ilipodhibitiwa.
Haijabainika vyema ni akina nani hasa walioshambulia lakini yamewahi kufanyika mashambulio kama hayo hasa katika maeneo ya wanajeshi wa angani na wa majini ambapo wanamgambo wa Taliban walihusika

Papa awapokea Peres na Abbas



Mahmoud Abbas, Papa na Shimon Peres Vatikani
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Francis amewakaribisha Rais wa Israil, Shimon Peres, na mwenzake kutoka Palestina, Mahmoud Abbas, katika maombi ya aina ya kipekee katika makao makuu ya Kanisa Katoliki ya Vatican. Viongozi hao wawili walikutana na Papa nje ya makaazi yake kabla ya kuandamana naye, wakiandamana na kiongozi wa Kanisa la Ordhodoz, Partriarch Artholomew kwa hafula maalumu katika Medani ya Vatican. Akiongea katika hafula hiyo Papa alisema ujasiri na nguvu vinahitjika katika juhudi za kuleta amani.
"Kuleta amani kunahitji ujasiri mkubwa kuliko vita. Kunahitaji ujasiri wa kusema ndio kwa mkutano na La kwa vita; ndio kwa mashauriano na La kwa makabiliano; ndio kwa kuheshimu mikataba na La kwa uchokozi; Ndio kwa ukweli na La kwa Uongo; kwa haya yote tunahitaji ujasiri na nguvu moyoni," Papa alisema
Na katika hotuba yake Bwana Peres alisema alitakia vizazi vyote vijavyo amani ya kudumu:

"Rafiki wapenzi, Nilikuwa mchanga, na sasa nimezeeka. Nilishuhudia vita, Nilionja amani. Sitawahi kusahau familia zilizofiwa, wazazi na watoto waliolipia gharama kubwa kwa vita hivyo. Na maisha yangu yote sitakoma kuitisha amani, kwa niaba ya vizazi vijavyo. Naomba sisi sote tuuungani mikono na kufurahi kwa sababu ni wajibu wetu kufanya hivyo kwa niaba ya watoto wetu.
Na kwa upande wake Bwana Abbas aliombea amani katika mkutano huo," alisema Peres.

Naye kiongozi wa Palestina, Mahmoud Abbas, aliomba kwenye hafula hiyo.

"Ee Bwana, tuletee amani ya kudumu na ya haki katika taifa letu na eneo letu, kwa ujumla, ili watu wetu na watu wote wa Mashariki ya Kati na Dunia nzima ifurahie matunda ya amani, utangamano na kuishi kwa pamoja kwa upendo.
Baada ya sherehe hiyo, iliyoshirikisha maombi ya Kikristo, Kiyahudi na Kiislamu, waliokuwepo walisalimiana kwa mikono na kupanda Mzaituni katika Medani ya Vatican kama ishara ya amani.
Papa ametangaza hadharani kuwa hataki kuingilia moja kwa moja mashauriano ya amani ya Mashariki ya kati, yaliyoporomoka Aprili lakini akasema kuwa anatarajia kwamba mkutano katika Vatican utapunguza uahasama kati ya pande hizo mbili kinzani za Mashariki ya Kati.

Friday, 6 June 2014

walioshiriki mbio za mita mia nne bonanza la ajtc hawa hapa

baadhi ya wanafunzi walioshiriki mbio za mita mia nne

kwa upande  wa wanawake ambao wameshiriki  wasichana nane na kuibuka msichana mmoja  kuibuka kidedea ambaye ni  editha mshana  na wasichana wengine kuishia njian.

 Hata hivyo  pia kwa upande  wa wavulana nao alipatikana mshindi ambaye aliwaacha kwa umbali mrefu ambapo alipatikana mshindi ambaye ni Ayubu martin aliyeibuka kidedea hapo jana.

mtawa anyakuwa ushindi wa uimbaji italia




Mtawa wa Italia anyakua ushindi


Mtawa mmoja kutoka Italia ambaye alipata umaarufu katika mtandao wa kijamii ameshinda shindano la kuimba nchini humo.
Mtawa huyo, Sister Christina Scuccia alitokea kwa mara ya kwanza katika

Ni uhalifu kuwanyanyasa wanawake - Misri


 


wanawake wa misri

Kwa mara ya kwanza Misri imepitisha sheria inayotaja unyanyasaji wa wanawake kuwa uhalifu.
Chini ya sheria hiyo wanaume watafungwa miaka 5 gerezani kwa kuwanyanyasa wanawake hadharani au faraghani.
Sheria hiyo imepitishwa kama hatua ya mwisho kuchukuliwa na rais anayeondoka wa Misri Adly Mansour.
'Unyanyasaji umezidi'
Watetesi wa haki za wanawake nchini Misri wamesema kuwa unyanyasaji wa wanawake umefikia viwango vya kuhuzunisha. Utafiti uliofanywa umeonesha kuwa karibu wanawake wote wa Misri wamewahi kupitia unyanyasaji wa aina fulani iwe ya matusi au hata ubakaji.
Utafiti huo umeonesha kuwa hata mavazi ya kufunika mwili wote yanayopendekezwa na sheria za kiislamu nchini humo, hazijawazuia wanaume hao kuwanyanyasa wanawake.
Na sasa inahofiwa kuwa mapinduzi waliofanya mwaka wa 2011 hayakuleta mabadiliko yoyote.
Wanawake wengi wamelalamika kuwa walinyanyaswa wakiwa katika maandamano katika midani ya Tahrir.
'Tatizo liko kwa itikadi mbovu'
Watetesi hao wa haki wanasema kuwa polisi mara nyingi wanawalaumu waathiriwa kuliko wale wanaofanya uhalifu huo.
Sasa sheria hii inachukuliwa kama hatua kubwa sana kusaidia tatizo hilo, ila hofu ni kwa utekelezaji wake. Wadadisi wanasema kuwa itakuwa vigumu zaidi kubadilisha itikadi za watu juu ya unyanuasaji wa wanawake nchini hum.

Thursday, 5 June 2014

fahamu Jinsi ya kuondoa harufu mbaya kwenye kwapa

Jinsi ya kuondoa harufu mbaya kwenye kwapa

G7 wakutana Brussels bila Urusi



mkutano wa G7

Viongozi wa mataifa tajiri ya magharibi wanaokutana mjini Brussels wamesema kuwa wako tayari kuweka vikwazo zaidi kwa Urusi iwapo itaendelea kuvuruga amani mashariki mwa Ukrain.
Taarifa ya pamoja ya mataifa ya G7 imesema kuwa Mambo yanayofanywa na Urusi nchini Ukrain hayawezi kubalika kamwe na lazima yakomeshwe.
Huu ndio mkutano wa kwanza wa viongozi hao tangu waifukuze Urusi kama mwanachama.
Urusi ilibumburushwa kutoka G7 kwa kosa lake kubwa zaidi, kuinyakua Crimea kutoka Ukrain.
Viongozi wa mataifa hayo ya G7 wanakutana sasa kwa mara ya kwanza tangu wakati huo.

Ukrain vita vimechacha
Lakini huku wakikutana mapigano yamechacha kati ya serikali ya Ukrain na majeshi yanayo unga mkono Urusi mashariki mwa Ukrain.
Urusi imeendelea kukana kuhusika na mapigano hayo. Miongoni mwa mikutano iliyopangwa Alhamisi hii, waziri mkuu wa Uingereza Davin Cameron atakutana na rais Obama mjini Brussels, ambapo kwa upana zaidi watazungumzia Urusi. Kisha baada ya mkutano huo, David Cameron ataelekea Paris Ufaransa kwa mkutano wa faragha na rais wa Urusi Vladmir Putin.

Katika wiki hii mataifa ya Uropa yamekuwa yakiadhimisha siku ya kuikomboa bara Uropa kutoka utawala wa ki Nazzi katika vita vya pili vya dunia miaka 70 iliyopita.

Huku hayo yakitokea, juhudi za kidiplomasia zimeshika kasi miongoni mwa mataifa ya magharibi kumaliza uhasama kati yao na Urusi.
G7 wamepongeza uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Ukrain na wameirai Urusi kumpokea na kushirikiana na rais mpya wa Ukrain Petro Poroshenko. Pia wameonya kuwa hawatasita kuiwekea Urusi vikwazo zaidi iwapo itakataa kusaidia kurejesha uthabiti Ukrain.
Itakuwa ni mara ya kwanza kwa miaka 17 ambapo G7 inakutana bila Urusi.

Bashar Al Assad ashinda uchaguzi Syria

Assad ashinda Uchaguzi
Maafisa nchini Syria wamesema kuwa Bashar Al Assad amechaguliwa tena kama rais wa nchi hiyo.
Assad amepata asili mia 89 ya kura zote. Uchaguzi huo umefanyika katika mazingira ya vita vya wenyewe kwa wenyewe na inaaminika kuwa wraia waliokuwa katika maeneo yanayoshikiliwa na serikali pekee ndio waliofanikiwa kupiga kura.
Upande wa upinzani ulisusia uchaguzi huo wakiutaja kuwa kejeli kwa demokrasia. Upande wa serikali hata hivyo umesema kuwa uchaguzi huo umepata kuungwa mkono na wengi zaidi waki kisia kuwa asili mia 73 ya raia walijitokeza kupiga kura.
Tnagu kutolewa matokeo hayo, wafuasi wa rais Assad wamekuwa wakisherehekea katika barabara za Damascus.
CHANZO BBC

Wampigisha kwata Waziri wa Afya



Waziri wa Afya, Dk Seif Rashid.0
Share


Wabunge wanawake bila kujali itikadi za vyama juzi usiku waliungana kuibana Serikali wakishinikiza iongeze fedha za Bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya mwaka 2014/15 ili kukabiliana na vifo vya kina mama na watoto.
Kibano hicho kilianza mapema asubuhi lakini moto zaidi uliwaka jioni wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha bajeti hiyo iliyotengewa Sh622 bilioni, ikiwa ni pungufu ya Sh131 bilioni ya bajeti ya wizara hiyo mwaka 2013/14 ambayo ilitengewa Sh753 bilioni. Wabunge wanawake 10 na wanaume wawili walichangia ikiwamo kutoa shilingi.
Kambi ya Upinzani ilianza kuibana Serikali ikisema imeweka rehani wananchi wake kutokana na kitendo chake cha kuchangia kiasi kidogo cha fedha za maendeleo za wizara hiyo.
Akiwasilisha taarifa ya kambi, Waziri Kivuli wa Afya, Dk Anthony Mbassa alisema Bajeti ya Sh622 bilioni na fedha za maendeleo ni Sh305 bilioni ambazo kati ya hizo, Serikali itatoa Sh54 bilioni tu, wakati washirika wa maendeleo watatoa Sh251 bilioni.
“Hii inaonyesha wazi kuwa Serikali imeendelea kuweka rehani wananchi wake kutokana na bajeti kuendelea kuwa tegemezi kwa wahisani,” alisema.
Kibano cha wanawake
Licha ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi, Waziri wa Afya, Dk Seif Rashid na Naibu Mawaziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na Adam Malima kutoa ufafanuzi, walishindwa kuwashawishi wabunge hao waliokuwa wakililia nyongeza ya bajeti.
Hoja hiyo, iliibuliwa na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Cecilia Paresso baada ya kuondoa shilingi akiitaka Serikali itoe majibu ya sababu za kutoa Sh387 bilioni pekee kati ya Sh753 bilioni za bajeti ya mwaka 2013/14, jambo ambalo limekwamisha utendaji kazi wa wizara hiyo, ikiwa ni pamoja ya kushindwa kutekeleza Azimio la Abuja kuwa kila nchi itenge asilimia 15 ya bajeti kuu kwa ajili ya Wizara ya Afya ili kunusuru vifo vya kina mama na watoto.
Baada ya kauli hiyo wabunge kadhaa walisimama na kuunga mkono hoja hiyo licha ya Mwigulu kulieleza Bunge kuwa Serikali imepanga kuongeza kiasi cha fedha kilichobaki kabla ya Juni 31, mwaka huu.
Hoja hiyo ilifafanuliwa na Malima ambaye alisema Serikali imetoa Sh12 bilioni na kwamba tayari fedha hizo zimeshaingizwa katika akaunti ya Wizara ya Fedha kwa ajili ya kulipia deni la Bohari Kuu ya Dawa (MSD), ambalo ni Sh89 bilioni na deni la matibabu nje ya nchi ambalo ni Sh21 bilioni.
“Kwa nini Bunge lilipitisha Sh753 bilioni wakati likijua wazi kuwa haziwezi kupatikana, Watanzania watapataje huduma za afya?” alihoji Paresso.
Jaji Werema alijibu akisema Azimio la Abuja ni la hiari na hata kama nchi husika ikishindwa kulitekeleza haitapata adhabu yoyote, huku akisisitiza kuwa Serikali haikupata fedha za kufikia malengo ya azimio hilo na kuahidi kuwa kiwango cha fedha kilichobaki kitaongezwa kabla ya mwisho wa mwezi huu.

Wednesday, 23 April 2014

KUTANA NA GINA KATIKA PISHI LA DAGAA LILILOPIKWA KWA MAFUTA YA MAWESE NA UGALI WA DONA

Haya  sasa  jamani  tunakutana  tena  katika  mambo  yetu  yale  ya  mambo  ya  maakuliiiiiii kila mtu haya  maeneo  anakuwa yupo makini  sana

WANAFUNZI WA SEKONDARI MTWARA WALALA SAKAFUNI


Wanafunzi  68 kati ya 556 wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Bweni katika Manispaa ya Mtwara-Mikindani, wanalazimika kulala chini kutokana na upungufu wa

Thursday, 10 April 2014

kutana na aunt gina katika kutambua Dalili za mwanaume anayekupenda kwa dhati


ANAVYOTAZAMA
Mwanasaikolojia Zick Rubin kutoka Chuo cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema kwamba watu wanaopendana hutumia asilimia 75 kutazamana kuliko