Wednesday, 23 April 2014

KUTANA NA GINA KATIKA PISHI LA DAGAA LILILOPIKWA KWA MAFUTA YA MAWESE NA UGALI WA DONA

Haya  sasa  jamani  tunakutana  tena  katika  mambo  yetu  yale  ya  mambo  ya  maakuliiiiiii kila mtu haya  maeneo  anakuwa yupo makini  sana
  huwa  hapendi  kupitisha  huu mda  na  kama  akipitisha  basi  ita  kuwa  ni  kwa  bahati  mbaya.

Leo twende  tukaone  pishi  la dagaa  waliopikiwa  mafuta  ya  mawese.  pamoja  na  ugali  wa  dona naamin utafurahi  sana  kuona  chakula  hiki na endapo  ukipika  nyumbani  mwako utakifurahia saaanaaaaaaaaaaaa

MAHITAJI
dagaa
nyanya
vitunguu
hoho
karoti
mafuta ya mawese
chumvi
unga wadona

JINSI  YA  KUANDAA
unachambua  dagaa wako  vizuri  unatoa  vichwa  na  wengine  huwa  hawatoi  vichwa  lakini  tunafanya  hivi  ili  kupunguza  michanga  nadagaa  pia  waweza  kupika  wa  wa mwanza  wale  wadogo  au  wakubwa  wa  kigoma

unaziweka  kwenye  kikaango  kwa  ajili  ya  kuwababua  kidogo  baada  ya  hapo  unaziweka  katika  maji  ya  uvuguvugu  lengo ni  kuziosha  na  kama  kuna  michanga  imebaki  kwenye  dagaa  huwa  inatoka  kwa  urahisi  wakati  wa  kuziosha  baada  ya  hapo  unaziweka  kwenye  bakuli  safi





unaweka  kiasi  cha  mafuta  kwenye  sufuria  ya  kupikia  unatenga  jikoni  kwenye  moto  yaanze  kuchemka  hadi  uone  povu  ila  hakikisha  hayabadiliki  rangi  yake ya  kawaida  ya  njano baada  ya  hapo  unakatia  kitunguu  pamoja  na  karoti pamoja  na  dagaa  unaanza kukoroga  taratibu  mpaka  uone  dagaa  wanaanza  kukauka  baada  ya  hapo  unaweka  nyanya  kwenye  huo  mchanganyiko  wako unasubili  kwa  dakika  chache  kisha mboga  yako  itakuwa  tayari  kwa  kuliwa  na  ugali  wako  wa  dona 

Siyo mbaya  ukanywa  na  juisi  yako  baada  ya  kula  chakula  chako  hicho

No comments:

Post a Comment